Friday, August 26, 2011

VODACOM TANZANIA NA MAONESHO YA SEKTA YA MAWASILIANO


Rais Dk.Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Meneja mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bw Salum Mwalim jinsi ambavyo Vodacom inavyochangia maedeleo ya vijijini kupitia teknolojia ya simu ya mkononi ikiwemo huduma ya m-pesa na MWEI huku akipitia jarida la Vodacom alipotembelea banda la kampuni hiyo katika maonesho ya wadau wa mawasiliano ya simu yanayofanyika sanjari na mkutano mkuu wa mwaka wa wadau wa sekta ya mawasiliano barani Afrika - CTO. jijini Dar es salaam ambao Vodacom ni mdhamini.


Rais Dk. Jakaya Kikwete akioneshwa na Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bw. Salum Mwalim fulana ya Vodacom yenye logo na rangi mpya za kampuni hiyo tangu ilipobadilika kutoka buluu kuwa nyekundu Aprili Mwaka huu wakati alipotembelea banda la kampuni hiyo katika maoensho ya sekta ya mawasiliano yanayofanyika sanjari na mkutano wa mwaka wa wadau wa mawasiliano ya simu barani Afrika jijini Dar es salaam jana ambao Vodacom ni mdhamini.
Mkuu wa Huduma za kifedha wa kampuni ya Vodacom Jacques Voogtz akiwasilisha mada juu ya njia za kusaidia maendeleo vijijini kupitia teknolojia za mawasiliano ya simu katika mkutano wa mwaka wa taasisi ya mawasiliano ya Jumuiya ya Madola - CTO unaofanyika jijini Dar es salaam. huduma ya m-pesa imekuwa mfano mzuri wa ukombozi wa kimawasiliano katika nyanja ya kifedha kwa wananchi vijijini hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

hostgator coupon code