![]() |
David Jairo akiwa Ofisini kwake jana baada ya kuripoti. |
Baada ya kutangazwa kurejeshwa kazini kwa katibu huyo, Wabunge walihoji uhuru wa mhimili wa Bunge na kuingiliwa katika maamuzi yake jambo lililozua mjadala na wabunge hao kutoa hoja bungeni ya kuundwa kwa Tume ya uchunguzi juu ya jambo hilo ikiwa ni pamoja na kuchunguza mambo mengine.
Furaha ya Jairo imedumu kwa masaa kadhaa tu baada ya kupokelewa kwa shangwe na ndelemo wakati alipowasili kuripoti ofisini kwake jana huku baadhi ya wafanyakazi wakimlazimisha kuzima gari lake na wao wakaanza kazi ya kulisukuma hadli mahala pa maegesho, huku waziri wake akifurahi kwa kurejea kwa Katibu huyo wizarani hapo ambapo alisema kuwa nashukuru Sheria imefuata mkondo wake kwa kutenda haki kwa Katibu huyo.
No comments:
Post a Comment