Wednesday, September 7, 2011

WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA BUNGE LA VIAJANA NCHINI LONDON


Wawakilishi wa vijana wa Tanzania katika Bunge la Vijana wakipozi kwa picha katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza baada ya kuwasili nchini humo kwa ajili ya kuwakilisha vijana katika Bunge hilo.

Ubalozi wa Tanzania Nchini Uingereza Kwa Kushirikiana na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamewateua Linda Kapinga na Lucy Minde kutuwakilisha katika mkutano wa nne wa Commonwealth Youth Parliament ( Bunge la Vijana) ulioanza tarehe 6-10 Septemba 2011 jijini London.

Wawakilishi hao wakiwa katika mahojiano.
Mkutano huo Umeandaliwa na Commonwealth Parliamentary Association tawi la Uingereza ikishirikishwa na Sekretarieti ya CPA ambayo ni Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Katibu wake ni Mwafrika wa kwanza kuteuliwa na Pia ni Mtanzania mwenzetu Dr William Shija.
Pozi la picha Ubalozini hapo.

No comments:

Post a Comment

hostgator coupon code