WATU wanne akiwemo nahodha wa meli ya mv Spice Islander wameshitakiwa katika Mahakama Kuu ya Zanzibar wakihusishwa na kuzama kwa meli hiyo Jumamosi alfajiri na kuua watu zaidi ya 200.
Nahodha wa meli hiyo, Said Abdallah Kinyanyite (58), msaidizi wake Abdallah Mohamed Ali (30), Ofisa Usalama wa Bandari ya Zanzibar, Simai Nyange Simai (27), na ofisa kutoka katika kampuni inayomiliki meli hiyo, Yussuf Suleiman Jussa (47), ndio waliopanda kizimbani.
Wanashitakiwa kwa makosa ya uzembe chini ya Kifungu 236 cha Sheria Namba 6 ya Zanzibar ya mwaka 2004. Hata hivyo, nahodha wa meli hiyo, hakuwepo mahakamani mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, George Kazi ambaye pia alikataa kutoa dhamana kwa washitakiwa wengine kama alivyoombwa na wakili wa utetezi Hamid Mbwezeleni.
“Hii ni kesi nyeti, nasita kukimbilia katika kutoa dhamana. Nitatoa uamuzi wangu kuhusu
maombi ya dhamana Jumatatu ijayo, hivyo naamuru washitakiwa warudishwe rumande,” alisema Msajili.
Washitakiwa hakuwatakiwa kujibu lolote. Mv Spice Islander ikiwa imesheheni mizigo na abiria kuliko uwezo wake, ilizama kilometa 10 kutoka pwani ya Nungwi wakati ikiwa njiani kwenda Pemba, usiku wa Septemba 9, mwaka huu.
Inaaminika kuwa wengi wa abiria 203 walikuwa watoto, waliokuwa wamelala chini wakati wa ajali. Hata hivyo, Tume maalumu itaundwa kuhusu ajali hiyo ambayo watu zaidi ya 600 waliokolewa.
Nahodha wa meli hiyo, Said Abdallah Kinyanyite (58), msaidizi wake Abdallah Mohamed Ali (30), Ofisa Usalama wa Bandari ya Zanzibar, Simai Nyange Simai (27), na ofisa kutoka katika kampuni inayomiliki meli hiyo, Yussuf Suleiman Jussa (47), ndio waliopanda kizimbani.
Wanashitakiwa kwa makosa ya uzembe chini ya Kifungu 236 cha Sheria Namba 6 ya Zanzibar ya mwaka 2004. Hata hivyo, nahodha wa meli hiyo, hakuwepo mahakamani mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, George Kazi ambaye pia alikataa kutoa dhamana kwa washitakiwa wengine kama alivyoombwa na wakili wa utetezi Hamid Mbwezeleni.
“Hii ni kesi nyeti, nasita kukimbilia katika kutoa dhamana. Nitatoa uamuzi wangu kuhusu
maombi ya dhamana Jumatatu ijayo, hivyo naamuru washitakiwa warudishwe rumande,” alisema Msajili.
Washitakiwa hakuwatakiwa kujibu lolote. Mv Spice Islander ikiwa imesheheni mizigo na abiria kuliko uwezo wake, ilizama kilometa 10 kutoka pwani ya Nungwi wakati ikiwa njiani kwenda Pemba, usiku wa Septemba 9, mwaka huu.
Inaaminika kuwa wengi wa abiria 203 walikuwa watoto, waliokuwa wamelala chini wakati wa ajali. Hata hivyo, Tume maalumu itaundwa kuhusu ajali hiyo ambayo watu zaidi ya 600 waliokolewa.
Uwezo wa meli hiyo ilikuwa ni kubeba watu 610. Katika hatua nyingine, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imetoa tamko la kusitishwa rasmi kwa kazi ya utafutaji wa miili ya watu walionasa kwenye vyumba vya meli ya mv Spice Islander kutokana na ugumu
wa utekelezaji wa kazi hiyo.
Kusitishwa kwa kazi hiyo kunatokana na kushindwa kwa wazamiaji wa kimataifa kutoka Afrika Kusini kuifikia meli hiyo kutokana na kina kirefu kilichopo eneo la ajali pamoja na hali mbaya ya hewa.
Akitangaza uamuzi huo wa SMZ, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd, alisema ingawa Serikali ilikuwa na nia ya kutaka kutolewa kwa kila miwili iliyonasa kwenye meli hiyo, lakini imeonekana kuwa kazi hiyo ni ngumu kutekelezeka.
Amewaomba Watanzania kukubali kuwa ndugu zao waliopoteza maisha na miili yao kushindikana kupatikana, ni mapenzi na uamuzi wa Mwenyezi Mungu aliyeamua kuwa bahari iwe sehemu ya makaburi ya ndugu zetu hao. Source Habari Leo
wa utekelezaji wa kazi hiyo.
Kusitishwa kwa kazi hiyo kunatokana na kushindwa kwa wazamiaji wa kimataifa kutoka Afrika Kusini kuifikia meli hiyo kutokana na kina kirefu kilichopo eneo la ajali pamoja na hali mbaya ya hewa.
Akitangaza uamuzi huo wa SMZ, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Idd, alisema ingawa Serikali ilikuwa na nia ya kutaka kutolewa kwa kila miwili iliyonasa kwenye meli hiyo, lakini imeonekana kuwa kazi hiyo ni ngumu kutekelezeka.
Amewaomba Watanzania kukubali kuwa ndugu zao waliopoteza maisha na miili yao kushindikana kupatikana, ni mapenzi na uamuzi wa Mwenyezi Mungu aliyeamua kuwa bahari iwe sehemu ya makaburi ya ndugu zetu hao. Source Habari Leo
No comments:
Post a Comment