Thursday, September 29, 2011

SPIKA WA BUNGE MAMA ANNA MAKINDA AMTEMBELEA DK MWANDOSYA HOSPITALINI NCHINI INDIA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Anna Makinda akimjulia hali Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya alipomtembelea katika hospitali ya Apollo nchini India ambako Profesa Mwandosya amelazwa kwa matibabu. Hali yake inaendelea vyema
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Seif Shariff Hamad akiwa katika mazungumzo na Prof. Mark Mwandosya na Bwana Rodhey Mohan, Meneja Mkuu wa Hospitali ya Apollo alipofika kumjulia hali Prof Mwandosya ambaye amelazwa hapo kwa matibabu baada ya kuhitimisha ziara yake India iliyomchukua katika majimbo ya Andhara Pradesh, Kerala na Karnataka.
 
Kutoka kushoto ni Mhe. Mohamed Aboud (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili, Zanzibar), Mama Lucy Mwandosya, Bw. Radhey Mohan, Meneja Mkuu wa Hospitali ya Apollo, Mhe. SEIF Shariff Hamad na Prof. Mwandosya

No comments:

Post a Comment

hostgator coupon code